Thursday, 24 September 2015

BAADHI YA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI BAADA YA MATOKEO YA UTAFITI WA TWAWEZA


Ni leo tena nikivipitia vichwa vya habari kwa Magazeti mbalimbali ya hapa Nyumbani. Hii ni baada ya Utafiti wa kikundi flani kinachojiita TWAWEZA kutoa kile kinachokiita Utafiti .

Gazeti la Mwananchi

Gazeti hili limekuja na kichwa cha habari kikionyesha kuwa Utafiti wa Twaweza umetoka na kupondwa vibaya sana na Wananchi pamoja na Wasomi hapa Tanzania. Wakamaliza chini na Picha kuuuuuuubwaaaa ya Lowassa akifanya mkutano huko Masasi. (Ujumbe umeeleweka)

Gazeti la Nipashe

Gazeti hili limekuja na habari kubwa yenye kichwa cha habari, "Utafiti waipaisha ccm" ktk kushadidia habari hiyo chini yake limeandika "Wasomi na Wananchi wauponda vibaya sana" Chini wakamalizia na picha kuuuuubwaa ya mkutano wa Lowassa huko Masasi (Ujumbe umesomeka)

Gazeti la Tanzania Daima

Gazeti hili limekuja na habari kubwa yenye kichwa cha habari "Bao la Mkono, Twaweza watoa Utafiti kuibeba ccm, Wananchi wasomi Wauponda kila kona ya Nchi" Chini wakamalizia na Picha ya Mafuriko ya Lowassa huko Masasi (Ujumbe umeeleweka)

Gazeti la Raia Mwema

Gazeti hili lenyewe ndo halijataka hata kuripoti upuuzi wa Twaweza. Lenyewe limekuja na kichwa cha habari kilichoandikwa kwa ufupi sana, "MSHITUKO" Chini ya habari hiyo kuna picha kuuuuubwaa ya Lowassa akifanya mkutano wake huko Masasi wananchi wakiwa wamejazana kama mchanga wa bahari ya hindi. (Ujumbe pia umeeleweka)

No comments:

Post a Comment